Myanmar yatoa msamaha kwa wafungwa.
Kamanda wa Polisi mkoani Pwani Absalom Mwakyoma amethibitisha tukio hilo ambapo aliwataja wengine wawili waliokufa katika ajali hiyo ni Issaya Mbaga (32) kondakta wa gari T 637 ASK na Musa Msasi (45) mkazi wa Iringa na wote walifariki papo hapo.


Amesema majeruhi wa ajali hiyo ni dereva wa Scania Elia Mhando ambaye amevunjika mguu wa kulia na kwa sasa amelazwa katika hospitali  teule ya Tumbi Kibaha kwa matibabu na kwmaba miili ya marehemu imehifadhiwa katika kituo cha Afya cha Chalinze wilayani Bagamoyo kusubiri ndugu kwa mazishi.


Mwakyoma amesema chanzo cha aajli hiyo ni gari aina ya Canter kujaribu kulipita gari lingine ambalo halikufanikiwa kufahamika  na kabla hajafanikiwa kulipita ndipo kwa mbele ilipotokea scania hilo na hivyo kugongana na uso kwa uso.


Katika tukio jingine Kamanda huyo wa Polisi Pwani amesema mkazi wa Kongowe wilayani Kibaha Fadhili Mrisho (62) amekamatwa kwa kosa la kukutwa na nyara za Serikali meno ya tembo vipande vinne vyenye uzito wa kg.15.1 vya thamani ya mili.1.1.


Tukio hilo limetokea majira ya saa 8.00 mchana jana katika eneo la shule ya msingi Kongowe na waliomkamata mtuhumiwa huyo ni maafisa wa maliasili wa kituo cha Kongowe kwa ushirikiano na askari polisi na kwamba  mzee huyo anatarajiwa kufikishw amahakamani wakati wowote.













 







































.
Radio Free Africa, all rights reserved 1995 - 2009