Kwa mjibu wa ofisa mtendaji wa kijiji cha Kabainja Yuda Karumo, wananchi wa kijiji hicho pia wametishia kutokushiriki katika uchaguzi mkuu ujao kama kijiji chao, hakitarudishwa katika kata yao ya zamani ya Butimba.
Alisema kuwa kata hiyo ilikatwa na kuzaliwa kata mpya ya Kasuguti ambako kijiji chao kilipelekwa na kwamba kijiji chao kiko mbali sana na makao makuu ya kata hiyo mpya na kuongeza kuwa kibaya zaidi katika zoezi hilo uongozi wa kata hiyo haukushirikisha uongozi wa kijiji hicho.
Alisema kuwa kijiji chao kilikuwa miongoni mwa vijiji sita ambavyo ni Kabainja, Kasuguti, Buzimbwe, Mwiseni, Bulamba na Ragata, vilivyokuwa vinaunda kata ya Butimba.
Aliongeza kuwa ukataji wa kata hiyo haukuzingatia jogorafia ilivyo, pamoja na miundombinu, kwani kijiji chao kingewekwa katika kata ya Butimba yenye vijiji vya Bulamba na Buzimbwe.
Alisema kuwa kilio chao hicho pia walikwishakifikisha kwa Rais Jakaya Kikwete, wakati alipopita katika wilaya hiyo akielekea wilayani Ukerewe.
Wakati huo huo waziri wa kilimo, chakula na ushirka Stephen Wasira, ameibuka mshindi katika kura za maoni za ubunge wa jimbo la Bunda kupitia tiketi ya chcmc hicho, baada ya kumbwaga mpinzani wake wa karibu Ginche Kisase.
Kwa mjibu wa taarifa za awali Wasira alipata jumla ya kura 16,866, ambapo Kisase alipata kura 5048.
Katika jimbo la Mwibara Mwenyekiti wa jumuyia ya wazazi wa wilaya ya Bunda, Kangi Ndege Lugora, alimbwaga aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Charles Kajege, kwa kupata jumla ya kura 7521, ambapo Kajege aliambulia kura 4894.