JAMII imetakiwa kujenga utamaduni wa kuyasaidia makundi maalumu yenye matatizo mbalimbali katika maeneo yao .
Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa kikundi cha wanawake wa kanisa la Pentekoste (FPCT) Singida mjini bibi Lesi Betheli kwenye hafla ya kukabidhi msaada kwa wafungwa 21 wa kike wanaotumikia kwenye gereza la wilaya ya Singida na wagonjwa wa hospitali ya mkoa.
Msaada huo zikiwemo sabuni za kufulia na kuoga, vinywaji, biskuiti na pipi ulitolewa na kikundi hicho kama sehemu ya kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.
Bibi Betheli amesema kuwa pamoja na kuwepo kwa makundi mengi maalumu wakiwemo watoto yatima, wajane, wazee, walemavu, wenye virus vya UKIMWI na wafungwa lakini jamii imesahau kabisa kutoa misaada na kuona kama sio jukumu lao.
Amesema si busara sana kwa wanawake ambao ni watu wenye huruma nyingi na mapenzi makubwa kwa binadamu wenzao,kuishia tu kusherekea maadhimisho ya siku yao kwenye mikutano ya hadhara pekee badala ya kuyakumbuka makundi mbalimbali yenye mahitaji.
Kutokana na hali hiyo amesema kuna haja kwa watanzania husani wanawake kukumbuka na kutekelezaji wajibu huo muhimu ili kuyafanya makundi hayo kuhisi kuwa yanatambuliwa, kuheshimiwa na kuthamini na jamii inayowazunguka katika maeneo yao.
Radio Free Africa, all rights reserved 1995 - 2009
Na Emmanuel Michael , Singida